Sunday, April 11, 2010

BONITE WAZIDI KUGAWA ZAWADI


Huyu alimchukulia mwanae Aman Makwao tiketi ya kwenda Sauz"


Mmoja wa washindi wa TV ,Teresia Massawe


Baadhi ya washiriki wa tukio hilo, Mbele ni Patrick Dereck wa Kili fm, Yusuph Mazimu (masanja Jr) wa Moshi fm na Bahati Mustapha wa Moshi fm wakipata ka-"tea" kidogo.


Vigogo wa Coca Kanda Bonite Moshi na Arusha wakijadiliana majambozi baada ya utoaji wa zawadi.

Saturday, April 10, 2010

WATATU WATWAA TIKETI ZA COCA KWENDA SAUZI

Kiwanda cha Bonite cha mjini Moshi leo kimetoa tiketi tatu kwa washindi waliobahatika kupata vizibo vya soda vyenye tiketi ya kwenda Sauzi kushuhudia kombe la dunia.

Pia imetoa zawadi za TV kwa washindi wengine sita. Waliopata tiketi za kwenda Sauz ni Saimon Makao wa Arusha, Aman Ole Mkwao mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es salaam(UD) na Mohamed Bashiri wa kisongo Arusha. walitwaa TV aina ya sony ni Julius zephania wa KCMC moshi, Haji kileo wa Stand ya Mboya Moshi, Teresia Masawe wa Longuo KCMC, Jovina Samuel Mwita,Robinson elius na Kelvin Robert


Viongozi wa kiwanda cha bonite cha mjini Moshi, Kuanzia kushoto HRM, Bw.Dominic Urassa, General manager wa Arusha,Bw. Mongola Segule, Meneja wa fedha Bw. Gidion Kaaya, General manager wa Bonite Moshi,Gilbert Uisso na Christopher Loiruki ambaye ni meneja mauzo, wakiwa katika zoezi la kugawa tiketi kwa washindi wa kweya pipa na coca cola watakaokwenda kushuhuida kombe la dunia nchini Afrika kusini.


Hawa ni baadhi ya washindi wa tiketi pamoja na TV kwenye promosheni ya kweya pipa na Coca-cola.

Meneja mkuu wa Bonite, Gilbert Uisso akiwaasa watu kunywa soda ya coca,fanta na Srite ili kujishindia zawadi mbalimbali zikiwemo TV, Tshirt, soda ya bure na tiketi ya kwenda kushuhudia kombe la dunia.


Mshindi wa TV,julius Zephania akikabidhiwa zawadi yake na meneja mauzo wa Bonite, Christopher Loiruki.


Saimoni Makao mkazi wa Mianzini Arusha akipokea mfano wa tiketi yake kwenda sauz toka kwa meneja wa fedha Gidion Kaaya





Saimon akiwa na Yusuph M. Mazimu(masanja Jr), mara baada ya kukabidhiwa tiketi yake ya kwenda Sauz

Saimo akishukuru kwa kupata tiketi ya kwenda Sauzi.

Friday, April 9, 2010

Liyumba kizimbani tena leo


Aliyekuwa Mkurugezi wa fedha na utawala wa Benki kuu ya Tanzania (BOT), Amartus liyumba akiondoka kizimbani leo Kisutu dar es Salaam

Mechi ya Simba vs yanga yaahirishwa mpaka April 18

Ebwana Shirikisho la soka nchini TFF leo imewekabayana watani wa jadi watacheza April 18 badala ya jpili keshokutwa April 11, kwa nini? mh ukweli ishu imekuwa tyt kidogo, vigogo hivi vinataka wakipige uwanja wa uhuru kwa sababu ya kukwepa makato mengi kama watakipigia kwenye uwanja wa Taifa.
Serikali inataka mechi ichezwe uwanja wa taifa, sasa mvutano huu umepelekea game hii TFF wasogeze mbele kupatikane muafaka. Unajua Mechi ikichezwa uwanja wa Taifa kuna asilimia 40 inaondoka kwenye makato ya uwanja na mambo mengine wakati uwanja wa uhuru ni asilimia 20 tu zinakatwa, zinazobaki vilabu vinaambulia pamoja na makato ya TFF.


Yanga Simba

Semina ya ukusanyaji wa Kodi Kilimanjaro


Meneja wa Mamlaka ya mapato, TRA mkoa wa Kilimanjaro, Bi. patience Minga(kushoto) akiwa na maafisa wengine wa TRA, Eliakimu nangale na Bi. Kekisha Mutatina, kwenye semina ya siku moja ya masuala ya ukusanyaji wa kodi. Semina hiyo imefanyika leo na kuwashirikisha waandishi wa habari wa mkoa huo na ilifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Mamlaka hiyo.


Baadhi ya wajumbe wa semina hiyo


Meneja wa TRA kilimanjaro, Bi. Minga

sikujua what is happening btn these people



Ilikuwa hivi ...sikuona jipya



Ikaja hivi, mbona poa hamna mbaya



mh baadae hivi, moyo ukaanza kwenda mbio kidogo



Ilipokuja hapa, nikasema labda??mapigo ya moyo na damu ikagoma kusafiri




eeh ilipofikia vihi,nikaacha kupiga picha nikawauliza kulikoni wenzangu?
ah mh kumbe nothing chaendela zaidi walikuwa wanamsimulia mtu stori flan, kwa hiyo walikuwa wanajaribu kumuonyesha na vitendo kabisa ili aelewe. Mlinishtua lakini wajameni


Thursday, April 8, 2010

Poleni Ndugu zetu... kikubwa Tujipange next time



Kama mmeniachia me nifanyaje sasa?si nafunga... Mdachi Arjen Robben akishangilia goli lililoiondosha Man Utd katika robo fainali ya champions ligi jana ndani ya old traford.


Hivi kuondolewa kwa timu za uingereza katika michuano hii, je ni kushuka kwa kiwango cha timu za ligi ya nchi hiyo?ama? maana ni mara ya kwanza katika misimu tisa kukosekana kwa timu ya Uingereza kwenye nusu fainali.



Liverpool waliondolewa hata hakujakucha, Chelsea akondolewa asubuhi, Man na Arsenal zimeondolewa mchana na kuwaacha Inter Milan, Barca, Lyon na Buyern wakiendela na safari ambpo wawili wataishia jioni mwingine atajitoma mpaka usiku.

Wenger ah unaniboa



Mh uliniuzi ila nakukubali kuwa haufai, umetuonyesha kuwa kuna watoto na mitoto katika soka



Mafans wa Arsenal tumekumiss sana Broza Henry.

Lilikuwa ni jambo la kukubali tu kwamba Barcelona ni wakali kuliko arsenal.Wamewazidi kila kitu kuanzia mbinu, uwezo na utaratibu tu wa uchezaji.. mbaya zaidi Messi alikuwa zaidi ya mchezaji katika game hiyo na zaidi ya mchezaji katika dunia hii.

Aliweza kuamua game yeye peke yake kwa kufunga mabao 4, lakini liko wapi suala la Arsenal Wenger, kocha wa Arsenal kuendelea na sera zake za kuwabeba vijana?me naona wenger anachokosea ni kushindwa kutofautisha kitu "Umri" na vipaji. Arsenal ikifungwa tu utasikia timu ni changa, ina vijana wengi, angalia kiungo kuna avarage ya miaka 21" hii bwana haisaidi kitu unazidi kutuumiza wapenzi na mashabiki wa The Gunners wenye kiu ya kuliona kombe baada ya kulikosa kwa miaka kenda.

Wenger umesahau kwamba timu zingine zina vijana wengi tu wa umri mdogo kama hao makinda wako, lakini wenzetu wana vipaji ndo mana pale, sio umri tu uliowaweka kwenye timu zao. Angalia Sturridge wa Chelse, kijana mdooogo kabisa, Messi aliyekutia aibu ni kijivulana tu, Raphaeli wa man kakijivulana tu, Pagto wa AC Milan, na wengine kibao vijivulana tu lakini vipaji wanavyo. Sipingi kwamba unao vijana wenye vipaji hapo lakini walipaswa kuchanganywa na waongozaji kuwapa mbinu za kusaka ushindi mambo yanapokuwa magumu. Msimu huu ukiondoa Liverpool iliyo hoi bin taaban, hujaifunga timu yoyote kubwa si kwenye ligi kuu wala champions ligi.

Umepigwa na Man nyumbani na ugenini tena vipigo vya aibu. Umepigwa na chelsea home and away, Man city kakulamba, barcelona ndo hivyo, sasa timu gani unayoiita bora kama uzitandiki timu kubwa, maana kipimo cha ubora wa timu imara ni kuzichapa timu kubwa.

Ningekuwa mimi ndo wewe Wenger ningenunua wachezaji wanne tu walio tayari sio watoto yaani kiungo mzuiaji mmoja wa ukweli (Melo), Mshambuliaji mmoja wa ukweli (Higuan ama Dzeko), beki wa kati mmmoja wa ukweli (Hangaland) na kipa yeyote kutoka ulaya ya mashariki. Aaah unaniboa Wenger hata kunenepa sinenepi mwenzio cuz of your team, nunua bwana wenye uwezo msimu ujao tufanye mambo na Messi asituchezee tena.

Monday, April 5, 2010

BANZA, SONYO WAKUMBUSHIA ENZI ZA TOT, WAFUNIKA PASAKA NA DOZEE MUSICA



Hii ilikuwa usiku wa jana kwenye ukumbi wa Aventure Africa Moshi , huyu ni Banza nyuma yake ni Waziri Sonyo kwenye Jukwaa moja na Dozee Musica. Ukweli walifunika sana na pasaka ilikuwa poa kwa waliohudhuria.


Waziri Sonyo , hapa anakumbushia kijikipande flan hivi nimekisahau alikiimba wakati huo yuko TOT..... enhee Ni masimango sijui nini nii.




Unamkumbuka Huyu? ni jamaa Flan aliwika sana na MVIKO SOUND, mwnzoni mwanzoni tu mwa miaka ya 2000, Tosha one... alikuwa na rap yake inasema..... eeee eee haiwezekani kuniachia miwaya haiwezekani eti kunidatisha haiwezekani, nae aliwaka na Dozee Musica usiku wa jana.




Kushoto ni Waziri Sonyo "mzee wa Tanga"kulia kwake ni shosti flan alikuaga bendi ya Bwagamoyo Sound ile ya Kocha wa dunia,Muumini Mwinjuma, anaitwa Asha yuko na Dozee musica kwa sasa na jana aliwasha moto Aventure.



Teh tehe Mshkaji wangu, Chepe alikuwa Bwii mbayaaa... alisakata kila ngoma iliyopigwa, kila songi lililopigwa, nakumbuka alisimama dk 3 tena alikuwa anahangaika kuwasha sigara yake hiyo mkononi. Huyu ni nyota wa soka wa timu ya soka ya Mkoa wa Kilimanjaro na timu ya daraja la kwanza ya Nyerere SC ya mkoani Kilimanjaro.

KASA YAIPIGA JEKI KILI MEDIA FOOTBALL CLUB


Ndo ndo ndo si chururu, kidogokidogo ndiyo mwendo, najua mwanzo mgumu, na kawia ufike.... jamani nawataarifu waandishi wa habari wa Mkoa wa Kilimanjaro wamepania kufanya mageuzi kwenye sekta ya michezo kwa kuanzisha timu za mpira wa miguu na mpira wa pete.

Lengo ni kurekebisha afya zao, kuleta mshikamano na umoja miongoni mwao baada awali Chama chao cha MECKI kukaribia kuwavunja shingo pamoja na kunenga uhusiano wa kimichezo na kijamii baina yao na makundi mengine ya jamii yaliyojiingiza katyika michezo.

Kwa upande wa timu ya mpira wa miguu,KILIMANJARO MEDIA FOOTBALL CLUB, hata kabla ya kuanza mazoezi, tayari wafadhili wameanza kuona uelekeo, tayari shirika moja lisilo la kiserikali linalojihusisha na mapambano dhidi ya Ukimwi kilimanjaro , KASA limeipiga jeki kwa kupatiwa vifaa vya michezo zikiwemo jezi na mipira... ama kweli "Nyota njema uonekana asubuhi"

Cheki hapa



Kaimu katibu wa Kilimanjaro Media Football Club, Nakajumo James akipokea jezi kwa niaba ya timu hiyo kutoka kwa kaimu mwenyekiti wa baraza la wazee Kilimanjaro, Ablallah kimweri, aliyekabidhi kwa niaba ya Mkurugenzi wa KASA, Faraji Swai..



Sio duaa ila ni shukurani toka kwa Nakajumo kwa niaba ya timu kwenda kwa vigogo wa KASA.


Hapa Nakajumo akimkabidhi jezi nahodha wa Kilimanjaro media football club, Dixon Busagaga, aliyepokea kwa niaba ya wachezaji wenzake.




Ziko poa.. kisimba simba..teh teh ila safi....hawa ni baadhi ya wachezaji wa timu hiyo, wakiwa katika uzi waliokabidhiwa na KASA... kutoka kushoto ni Rodrick Mushi, Nakajumo, Busagaga, Kija na Zephania



Tehe teh aapa wapo katika pozi jingine, bila shaka pozi hili ni ubunifu wa Naka.. ila kiukweli jezi ziko poa sana, kazi kwao.

Saturday, April 3, 2010

Wazee wa masauti walivyotisha Mo town usiku wa kuamkia leo

Acudo Impact wazee wa masauti bwana walifanya mambo makubwa sana pande za moshi, ilikuwa Aventure Club Africa usiku wa kuamikia leo, show ilianza saa tatu flan hivi licha ya lijimvua na kukatika kwa umeme kutaka kuharibu show, wachaga na sii wakuja tuishio huku moshi, tukaona isiwe tabu tukachukua mijitax na mijigari yetu tukajitoma Aventure.

Show ikaenda sawa, watu walijaa na kuinjoy vya kutosha, ndugu zetu wa Tanesco wakaturudishia umeme wetu muda mfupi baadae, na jamaa wakasevu mafuta ya jenereta.
Ila ishu ikaja kama kuharibika hiv mwishoni mwa show, baada ya marapa mahiri wa bendi hiyo,
canal top na totoo ze bingwa kuchapana na kusabaisha canal kuvunjika mkono...so soooory canal




Ramadhan Masanja a.k.a Banza ama masanja seniour kushoto akiwa na Masanja Jr ndani ya studio za Moshi fm, kilimanjaro. Huyu ni mtu na mdogo wake....





Presenter wa Moshi fm Masanja Jr kushoto na rapa mahiri wa acudo Impact na nominee wa kili award this year,Totoo ze Bingwa



Mwimbaji wa Acudo Impact Tarsis Masela akiwa katika poooz na presenter wa Moshi fm masanja jr kabla ya kuanza kwa interview kwa ajili ya show ya ijumaa kuu ndani ya Aventure Africa moshi.




Tarsis, Banza, masanja jr na Totoo ze bingwa wakimsikiliza presenter upande wa pili wa studio za moshi fm.




Banza mtoto wa Bit jeberi, akihojiwa na mtangazaji Ntory mayombola, ambaye haonekani pichani




Banza, Masela na Totoo ze bingwa




Huyu dada alitia fora, kwanza wezere, pili kivazi, tatu jiumbo...mh kweli alikwenda show, akacheza show...aka..ka..aka... na kuk...ka...ti...ka katikatikati...alitishaaaa ukumbini kwa kila kitu.... nina clip yake jamani...anaetaka anicheki katika masanja80@yahoo.com




christian bella katikati akiongoza mashambulizi jukwaani




Inadaiwa mwishoni mwa show, Rapa huyu mahiri wa acudo Canal top, alivunjika mkono baada ya kutokea vurumai kati yake na Totoo za bingwa. Kisa mh.....sijui labda nanii..lakini yadaiwa ni ishu zao za kuraprap, mara huyu anaiingilia nikirap mara huyu anajiona mkali kuliko mwengine, mara oh ilimradi tu yakatokea yakutokea pale Aventure.





Shemeji yatu (mwenye red) akiwajimwaya na wanazi wengine wa Acudo



Kaka yake banza katikati Hamisi masanja pia alikuwepo Aventure

Friday, April 2, 2010

which pair is looking more swagaz????

'Big Poz' from the hook Presenter mazimu a.k.a Masanja Jr and kimodo cha ukweli Glory


Technician Sir Uroki pamoja na Lucy Wezere katika pozi mwananana na la maana


Kama sio wao vile.... Wamilazo & Hellen wapare wanajisifu kuwa nao, ni masupa star wakipare


Teh teh hamfundishi kumix ila ni pozi tu la kijob kutoka kwa Dj Clever & mrembo Re Junior